8 Novemba, 2012 - Saa 15:43 GMT
Shughuli za uokoaji ili
kutafuta manusuru zingali zinaendelea katika jengo lililoporomoka
jijini Accra, mji mkuu wa Ghana.
Jengo hilo, lililokuwa na orofa kadhaa,
liliporomoka siku ya Jumatano. Jengo hilo lilikuwa limekodishwa na duka
la Melcom, na lilifunguliwa mapema mwaka huu.Hadi sasa watu watano wamethibitishwa kufariki, huku wengine 65 wakiokolewa wakiwa hai.
Rais John Dramani amesitisha kwa muda kampeni zake za urais, huku akitangaza eneo la tukio kuwa eneo la janga. Pia, aliamuru uchunguzi kuhusu kilichosababisha mkasa huo, ufanywe.
Kikundi cha Waisraeli kinategemewa kuwasili Alhamisi ili kusaidia katika juhudi hizo za uokoaji. Wanategemewa kwamba watakuja na vifaa maalum pamoja na mbwa wa uokoaji.
No comments:
Post a Comment