Thursday, November 8, 2012

Shughuli za uokoaji zashika kasi Ghana

8 Novemba, 2012 - Saa 15:43 GMT

Shughuli za uokoaji zashika kasi Ghana
Shughuli za uokoaji ili kutafuta manusuru zingali zinaendelea katika jengo lililoporomoka jijini Accra, mji mkuu wa Ghana.
Jengo hilo, lililokuwa na orofa kadhaa, liliporomoka siku ya Jumatano. Jengo hilo lilikuwa limekodishwa na duka la Melcom, na lilifunguliwa mapema mwaka huu.
Mwandishi wa BBC, Sammy Darko, anayeripoti kutoka eneo la tukio, anasema anaona mikono ya watu watatu ikitokezea kutoka maporomokoni, huku waokoaji wakijitahdidi kuwafikia.
Hadi sasa watu watano wamethibitishwa kufariki, huku wengine 65 wakiokolewa wakiwa hai.
Rais John Dramani amesitisha kwa muda kampeni zake za urais, huku akitangaza eneo la tukio kuwa eneo la janga. Pia, aliamuru uchunguzi kuhusu kilichosababisha mkasa huo, ufanywe.
Kikundi cha Waisraeli kinategemewa kuwasili Alhamisi ili kusaidia katika juhudi hizo za uokoaji. Wanategemewa kwamba watakuja na vifaa maalum pamoja na mbwa wa uokoaji.

No comments:

Post a Comment